PIGA KURA BSS 2ND CHANCE; ANDIKA BSS 05 KISHA TUMA KWENDA NO. 15747.

Tafuta hapa

Friday 1 July 2011

KUTOKA MAGAZETINI

AGNES: Napenda nikiwa faragha na mpenzi wangu wote tuwe bwiii


Wiki hii kupitia safu hii tunaye sistaduu ambaye ni msanii wa filamu. Licha ya usanii, pia mwanadada huyu amejipatia umaarufu kutokana na kuuza sura kwenye video za mastaa mbalimbali wa muziki hapa Bongo. Anaitwa Agnes Gerald (pichani).

Alizaliwa Aprili 23, 1988 kwenye hospitali ya Mkoa wa Mbeya na akasoma Shule ya Msingi na Sekondari ya Sangu. Hayo ni kwa uchache tu, zaidi kuhusu Agnes, ungana nami katika maswali 10 niliyomuuliza.

TQ: Hili zali la kuuza sura kwenye video mbalimbali umelipataje? Kuna mtu yeyote ambaye anakuunganisha na wasanii hawa?
Agnes: Kwanza ni muonekano wangu lakini pia rafiki yangu mmoja alinikutanisha na baadhi ya wasanii hao na wao wakaona nafaa kuwemo kwenye kazi zao.

TQ: Inasemekana umetokea kwenye familia ambayo imeiva kidini, wao wanachukuliaje hili suala la wewe kuingia kwenye mambo haya ya kuuza sura tena wakati mwingine kwenye mavazi ya kimitego?
Agnes: Mh! Baba yangu hataki kabisa kusikia mambo ya muziki na niliwahi kukosana naye lakini nalazimisha kwa kuwa ni moja ya ajira.

TQ: Mbali na kazi ya kuuza sura, una dili nyingine zinazokuongezea kipato na kuweza kuishi mjini bila wasiwasi?
Agnes: Mimi ni mjasiriamali, nina teksi zangu mbili lakini pia katika siku zijazo nina mpango wa kufungua Super Market.

TQ: Vipi ‘outings’ zako, unapendelea kwenda sehemu gani?
Agnes: Napenda sana kwenda Club kujirusha hasa siku za wikiendi.

TQ: Kuna za chini chini kuwa umewahi kumlegezea Belle 9, hebu funguka katika hili.
Agnes: Siyo kweli bwana, huu ni mtambo mkubwa, mimi na yule wapi na wapi?

TQ: Kabla ya kuanza mechi ya kiutu uzima, unapenda wewe na mpenzi wako muwe katika hali gani?
Agnes: Huwa ‘nainjoi’ sana wote tukiwa tumelewa (Anaangua kicheko).

TQ: Ni kipi unachokumbuka katika mapenzi yako ya utotoni?
Agnes: Ni pale nilipokutana kwa mara ya kwanza na mwanamume. Pia nilipobeba ujauzito nikiwa mdogo hali iliyonifanya nifukuzwe nyumbani na baba.

TQ: He! Sasa ulijifungua au uliichoropoa mimba?
Agnes: Ilibidi nizae, tena mtoto wa kike, anaishi na baba yake huko Kinondoni ngoja nikuoneshe picha (Anafungua simu na kumuonesha mwandishi).

TQ: Dah! Mzuri sana, kwa nini huishi naye?
Agnes: Baba yake amemng’ang’ania kitu ambacho kimenifanya nimchukie mzazi mwenzangu huyo.

TQ: Lakini bado unampenda mwanamume huyo?
Agnes: Hapana kwa kuwa baada ya kunipa mimba alinisaliti, wakati nilifukuzwa nyumbani kwa sababu yake, kimsingi sitaki hata kumsikia.

GLOBAL Ujauzito wa Teddy Kalonga!

Na Mwandishi Wetu
Mwanadada aliyewahi kuwa Mtangazaji wa Televisheni ya Channel 5 kisha akapata zali la kuolewa na Mzungu nchini Marekani, Teddy Kalonga ‘TK’ (pichani)  amewashangaza mashabiki wake kufuatia kuanika picha yake ikionesha kuwa ni mjamzito.

Picha hiyo ambayo pia inapatikana kwenye blog yake inamuonesha TK ambaye pia anajishughulisha na ‘umodo’ akiwa na ‘kitumbo’ ambacho kwa haraka kinaonekana kuwa na zaidi ya miezi minne.

Wakiuzungumzia ujauzito huo, mashabiki mbalimbali wa mwanadada huyo walimpongeza kwa hatua hiyo lakini wakamlaumu kwa kuwaficha hadi mimba yake kuwa kubwa.

“Mimba imempendeza sana lakini mbona katuficha sisi wadau wake? Mungu amjalie ajifungue salama na ikiwezekana apate mapacha,” alisema Karen wa Moshi.

Naye Miriam Simbeyu wa Kinondoni jijini Dar alisema: “Nami sijui nitakuwa lini kama alivyo TK, mimba ni kitu kizuri sana hasa kwa walio katika ndoa…furaha ilioje kwake.”

Staa wa Kiwanda cha Filamu Bongo, Irene Uwoya ambaye hivi karibuni alijifungua mtoto wa kiume, ametoa somo kwa wasanii wenye majina makubwa nchini, kuacha tabia ya kutoa mimba kwa sababu kitendo hicho siyo kizuri, Ijumaa linashuka na mkoba wenye ishu nzima.

Akizungumza na gazeti hili katikati ya wiki hii nyumbani kwao Mbezi, jijini Dar es Salaam alipotembelewa na mwandishi wetu, Irene alisema anamshukuru Mwenyezi Mungu aliyewajalia kupata mtoto huyo ambaye amewatengezea heshima kubwa.
“Kusema ukweli mimi na mume wangu tunamshukuru sana Mungu, ametupa mtoto huyu, naamini amesababisha kuongezeka kwa heshima katika jamii,” alisema Uwoya.

Akaongeza: “Kwa wale wenzangu watoa mimba, nataka wajue ni hatari sana kwani wanaweza kupata matatizo, likiwemo la kutozaa kabisa maishani mwao.”

Aidha, aliongeza kuwa mwanamke anapozaa hupata heshima katika jamii inayomzunguka kwani anaitwa mama, jambo ambalo ni jema.
Irene aliongeza kuwa, kitendo cha kuzaa kinamfanya kuongeza ubize na shughuli za utafutaji wa ‘pesa’ ili kuongeza kipato kwa ajili ya kumlea mwanaye tofauti na mwanamke ambaye hana mtoto.

Akiendelea kutoa ushauri huo, alisema kwamba ikitokea mwanamke akapata ujauzito ambao hakuutarajia asithubutu kuutoa licha ya misukosuko atakayoipata na kuonekana asiyefaa.

“Unajua inapotokea msichana kapata mimba kabla ya kuolewa au akiwa shuleni, ndugu, jamaa na hata jamii itamuona mkosaji lakini hiyo isiwe sababu ya kuitoa kwani mtoto anapozaliwa hupendwa na kila mtu,” alisema Irene.
Kufuatia ushauri huo, Ijumaa liliwaendea hewani baadhi ya mastaa na kuwaambia ushauri huo wa Uwoya na kusikia kutoka kwao ambapo wa kwanza kutoa maoni alikuwa mtangazaji wa runinga Bongo, Maimartha wa Jesse ‘Mai’.

Yeye alisema: “Nikiwa mwanaharakati wa mambo ya wanawake nakubaliana na Uwoya, siwezi kutoa mimba hata siku moja kwani najua madhara yake.”

Mai aliyataja baadhi ya madhara hayo kuwa ni kulegea kizazi au kuharibika kabisa, kuvuja damu kila wakati (internal bleeding), kujiharibia maisha hasa pale unapoingia kwenye ndoa, mwanaume anataka mtoto wewe tayari umeshaharibu kizazi.

Mwanaidi Suka ‘Mainda’;
“Binafsi sijawahi kutoa mimba na sitathubutu kufanya hivyo kwani madhara yake ni kifo, kupoteza fahamu au kutokwa damu nyingi na pia ni kosa la jinai, nawashauri wenye tabia hiyo waache.”

Rehema Fabian, Balozi wa Kiswahili;
“Ukweli nakiri mimi niliwahi kutoa  mimba, lakini roho iliniuma sana nikizingatia kwamba, kitendo hicho kinaweza kusababisha kansa ya kizazi au ugumba. Sababu kubwa iliyonisukuma kufanya dhambi hiyo ni kugundua mwanaume mwenyewe hakuwa na msimamo, nikahisi nitailea peke yangu.”

Rose Ndauka;
“Kwa kweli mimi siyo daktari, siwezi kujua madhara ya kutoa mimba, ila kama mtu kanasa bila kutarajia siyo vibaya kuitoa ili asije akazaa mtoto ambaye atakuja kuteseka duniani.”
Naye supastaa mmoja wa filamu Bongo (aliomba jina lake lisitiriwe ili asijenge bifu na Uwoya) alisema kuwa, anamshangaa sana Uwoya kutoa somo hilo wakati na yeye ni staa.

“Heee! Makubwa! Uwoya ndiyo anasema hivyo? Naye si staa? Ina maana anatoa darasa hilo kwa sababu amepata mtoto, nina hakika hata yeye alishawahi kuchoropoa mimba kabla hajaolewa.
“Tusidanganyane, hapa Bongo hakuna staa wa kike ambaye hajawahi kutoa mimba kabla hajaolewa,” alisema staa huyo.

No comments:

Post a Comment