PIGA KURA BSS 2ND CHANCE; ANDIKA BSS 05 KISHA TUMA KWENDA NO. 15747.

Tafuta hapa

Sunday 10 July 2011

AJIFUNGUA MAPACHA WATANO KWA MPIGO

Bimbo akiwa na mapacha wake sita nchini Uingereza.
....Kabla hajajifungua.
MWANAMKE mmoja raia wa Nigeria, alipotambua ana ujauzito, aliamua kwenda Uingereza akitegemea watoto wange wangepata uraia wa nchi hiyo.

Hata hivyo, baada ya kujifungulia huko, mamlaka za Uingereza zimepinga kutoa uraia kwa watoto hao, licha ya kuwa alifaidika kwa kuhudumiwa akiwa hospitali na mfuko wa bima ya afya.

Mamlaka zilisema kwamba watoto wa mwanamke huyo, aitwaye Bimbo Ayelabola, (33), hawana haki ya moja kwa moja kuwa raia wa Uingereza, licha ya kuzaliwa nchini humo.

Kwa mujibu wa utaratibu huo, mamlala zilisema ili kupata sifa hiyo, mmoja wa wazazi wa watoto hao angekuwa raia wa Uingereza.

Muda wake wa kuishi Uingereza umemalizika Juni 27 mwaka huu  na kwamba anaweza kuongezewa muda wa miezi mingine sita ya kuishi humo. Hata hivyo, Bimbo ameamua kulifikisha suala hilo mahakamani akisema uamuzi wowote wa kuwazuia watoto wake kupata uraia utakiuka Sheria ya Uraia wa Uingereza iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2009.

Wakili wake alifafanua kuwa kipengelea cha sheria hiyo kinawalinda watu na kuwaruhusu kupata uraia kwa misingi ya kiafya.

Bimbo alikuwa akimeza dawa za kuongeza nguvu alipokuwa nyumbani kwao Lagos, Nigeria, kabla ya kuamua kwenda Uingereza ambapo alipatiwa huduma ya bima ya afya ya dharura akitegemea kujifungua watoto wanne.

Baada ya kujifungua watoto wanne, madaktari waligundua alikuwa na mtoto mwingine wa tano.

Mwanamke huyo ametuma maombi Wizara ya Mambo ya Ndani aongezewe muda wa kuishi Uingereza kwani afya za watoto wake hazijaimarika.

Mapacha wa Bimbo ni Yaseed na Samir, ambapo wa lkike ni Aqeelah, Binish na Zara ambao anasema hawawezi kupata msaada wa kuwalea kutoka kwa ndugu na marafiki zake ambao wengi wapo Uingereza.

Mumewe aitwaye Obi (37), alikwenda Uingereza kumwona akiwa hospitali na alipogundua ana ujauzito wa mapacha, alirejea Nigereia.

Wizara ya Mambo ya Ndani inasubiriwa kuona kama itamwongeza muda mama huyo, na inasemekana inatarajia kumpelekea ankara za huduma alizopewa mwanamke huyo hospitali.

Bimbo amesema hana uwezo wa kulipia ankara hizo na sasa anasaidiwa na Stella (26) rafiki yake waliyekuwa naye tangu shuleni ambapo kila mtoto anahitaji huduma za Pauni 70 kila wiki.
.....Akifikiria mustakabali wake baada ya kuambiwa atarejea kwao Nigeria.

Tuesday 5 July 2011

SHOW YA MACHOZI BAND JUMAPILI YA WIKI HII


?????????????/////
lady jay dee akiwa na warembo

Mr.shombeshombe aka SHAROBARO PRESIDENT nae alikuwepo





Hapa nikiwa naMachozi band tukishusha burudani



Good Pipo, Good Music, Nice Place
Picha zote kwa hisani ya ladyjaydee.blogspot.com

TOMBOY QUEENS; Pulling it off with the sexy boyish look

The rise of fashion  has broken all the rules. Who said being a sexy tomboy involves long torn jeans and sluckish wide t.shirts. Gals all you have to do is sex the look up like these sex dripping babes and you’ll have a score to die for.
You can hit back to the 80's with sexy boyish caps like these
Showing some flesh always sexies up your look
Check me out; sexy checked shorts like these are known to enhance the hips wider

Monday 4 July 2011

MWANAMUZIKI KUTOKA UGANDA CINDY AJIFUNGUA


Cindy with daughter
Weeks after dropping tot, city Diva Sanyu Cinderella aka Cindy is set to jet out with her Italian born fiancĂ© Mario Brunettes. The mission is simple; to visit her fiancĂ©’s parents and relatives plus to show them her new born baby girl. A close pal to the Ayokyayokya singer intimated to us;
“She is excited because she is now part of the family. They love her and they want to meet their grand daughter. She will jet out soon.” Cindy is still recovering at home after a much publicized pregnancy gave way to a healthy baby girl at Case Hospital on Buganda Road, Kampala. The baby was named Amani, which the Ayokya yokya singer said she chose for its meaning which is Swahili for ‘Peace’.
.

BONGO STAR SEARCH 2011 HII HAPA

Bongo star search 2011,inakuja kwa kishindo kikubwa kwa kuwapa nafasi nyingine washiriki waliopita ambayo itakuwa na jina la BSS 2ND CHANCE. Mchuano utahusisha washiriki wa Bongo star search Kutoka mwaka 2006 hadi 2010.

image
Bongo star search 2011,inakuja kwa kishindo kikubwa kwa kuwapa nafasi nyingine washiriki waliopita ambayo itakuwa na jina la BSS 2ND CHANCE. Mchuano utahusisha washiriki wa Bongo star search Kutoka mwaka 2006 hadi 2010.

Historia ya Bongo star search
Bongo star search ilianza mwaka 2006,ambapo iliweza kuwapa nafasi vijana wa kitanzania wenye vipaji vya kuimba mziki,Azimio Hili la BSS limeweza kuleta mafanikio makubwa ya vijana wa kitanzania kwa muda wa miaka mine sasa.Kutoka mwaka 2006 mpaka 2010 BSS ilichukua ziara mikoa mbalimbali ya Tanzania kwaajili ya kutafuta Vipaji vya mziki.Washindi wa Bss miaka mine(4)iliyopita walipata zawadi nono ambazo ziliwasaidia kunyanyua mfumo wa maisha yao.

Mafanikio ya BSS kutoka mwaka 2006-2010
Bss imeweza kufanikisha hazma yake ya kutimiza ahadi zake kwa kutoa zawadi zote kwa washindi wa BSS miaka yote,na mafanikio hayo yamepelekea washindi kubadili mfumo wa maisha yao ,kwa ujumla.Pia zawadi zimekuwa zikiongezeka kila mwaka kuanzia BSS ilipoanza hadi sasa.

Maandalizi ya Bongo star search
Kila mwaka Bongo star search imekuwa ikifanya mchujo kwa kuchukua washiriki mbalimbali kila mkoa Tanzania na kutafuta vipaji vilivyo bora kabisa.
Mwaka 2011,majaji wa Bongo star search walikaa chini na kupitia mikanda yote ya BSS ZiliZopita toka mwaka 2006 hadi 2010,na hatimaye kuwapata washiriki 30 ambao walikuwa na vipaji vizuri zaidi.
Muundo wa Bongo star search 2011

Washiriki watakuwa thelathini(30)na watachukuliwa kutoka mwaka 2006 hadi 2010.
Kutokana na mfumo huu,Bss imeamua kuchukua washiriki waliofanya vizuri zaidi katika kila mwaka.

Malengo.
Malengo ya Bongo star search 2011 ni kuwapa nafasi nyingine washiriki wa miaka ya nyuma yaani 2ND CHANCE na kuwafanya wajulikane kwa mara nyingine,Pia watambulike kuwa wana vipaji ambavyo vinaweza kuwa hazina ya nchi yetu ya Tanzania.

Mipango ya BSS 2011
Benchmarkproductions mmiliki wa Bongo star search,imeamua kuleta mabadiliko katika Bss mwaka huu 2011.kwa kuwapa washiriki wa miaka iliyopita nafasi nyingine ya kuonyesha vipaji vyao na pia kuwaonyesha Tanzania kuwa bado tunavipaji ambavyo vilizalishwa na BSS miaka ya nyuma na bado havijapata nafasi ya kuonekana.

Kwa mara nyingine,washiriki wa Bongo star search 2011 watakuwa 30(thelathini)na watachujwa mpaka kufikia 14 kwaajili ya mipambano ya michujo ya kila wiki.
1. Kutakuwa na ufunguzi wa Bongo star search 2011 ambao utahusisha mafanikio ya BSS kutoka miaka mine (4)ya nyuma hadi sasa,Lengo ni kusheherekea Miaka mitano ( 5 )ya Bongo star search na pia miaka hamsini (50)ya Uhuru wa Tanzania
2.Hatutakuwa na usahili mwaka huu kwasababu tutawachagua washiriki wa BSS miaka ya nyuma kutoka 2006 hadi 2010.Hivyo badala yake tutafanya usajili wa washiriki 30 ambao watarushwa kwenye televisheni ya ITV kwa muda wa wiki mbili(2)baada ya hapo wananchi watawapigia kura washiriki 20 tu ili kuingia kwenye michuano
3.Baada ya kupata kura za washiriki 20,watapelekwa kwa majaji watatu(3)wa Bongo star search ambao watachujwa na kupatikana washiriki 14 ambao wataingia kwenye nyumba tayari kwa mashindano ya kuchujwa kila mwisho wa wiki
4.Kutakuwa na matukio mbalimbaili katika maandalizi ya Bongo star search kama,Press release na washiriki thelathini(30) watarushwa kwenye vyombo vya habari na magazeti kwaajili ya kutoa hamasa za kura kwa washiriki hao
5.Mapema Baada ya mchujo wa pili wa washiriki,ambao watakuwa 14,na watakuwa na mafunzo mbalimbali ambayo yatakuwepo kwa muda wote huo wa mashindano.mafunzo hayo ni kama, usafi,na Mziki.
7.Kutakuwa na vipindi 14 vya Bongo star search ambavyo vitakuwa vinaoneshwa kila wiki,ambapo kutafanyika mchujo kwa kila wiki.
8.Mashindano ya mwisho yatahusisha washiriki wanne (4)tu ambao watachuana vikali LIVE stajini ambapo watakuwa wakichujwa mpaka kupatikana mshindi wa kwanza(1)
9.Washindi watatu watapewa zawadi ,na mwaka huu zawadi ya mshindi wa kwanza itakuwa nono zaidi ya miaka mine (4)iliyopita
10.Mfumo wa kura wa Bongo star search Kila mwaka ni, Kura za majaji ni asilimia 60,na wananchi(wapigakura)ni asilimia 40.
11.Faina

NINI HATMA YA PETER MSECHU TPF ALLSTARS MWAKA HUU?


The Tusker All Stars TV show debut on Sunday night and millions of viewers across East Africa were reunited with 8 former Tusker Project  Fame stars all on one stage.
The Tusker All Stars set was also revealed on the night with a replica of the sun and its rays against a backdrop of numerous stars thus setting the stage for the unveiling of an amazing display of talent.
The opening performance was the stars own rendition of the Tusker Stand Tall theme song that was unveiled during the launch of the new look Tusker bottle.
During the show, the stars performed signature tunes of their favorite performers trying to woo viewers with their own version of the songs.
Styled by Connie Oluoch, the 8 stars; Hemedy, Ng’ang’alito, Patricia, Alpha, Msechu, Amileena, Davies and Caroline, performed songs by music icons such as Brenda Fassie, Kidum, Eric Wainaina and Sauti Sol.
Hemedy, Tusker Project Fame season two’s “casanova”, performed J- Boog’s “Let’s do it again while Season 3′s Patricia Kihoro performed a soulful rendition of Sauti Sol’s “I’m coming home” off their sophomore album, Sol Filisofia.
Carolyne, the dancing queen from Uganda, sang “Nakupenda” by the late musical Icon, Brenda Fassie.  Ng’ang’alito was another pleasant surprise as he broke the mould and performed legendary neo soul track, “No other love” by John Legend.
Amileena performed one of Africa’s best loved and renowned songs “Jabulani” by PJPowers while Msechu did his own version of Kidum’s “Mapenzi”.
Alpha showed his versatility by performing Eric Wainaina’s runaway hit, “Ritwa Riaku. Davis was the last on stage with his energetic rendition of Papa Wemba’s “Yollele”.
Viewers were also introduced to two Tusker All Stars Super Fans; Arjun, popularly known as Vipul and radio presenter Joey Mathenge.
The super fans, both avid followers of previous editions of Tusker Project Fame and keen music fans, shared their views on each of the stars performances while offering support to the stars.
Viewers from Kenya, Uganda, Tanzania and Rwanda will vote for the top 3 stars during the 8 week reality TV show.
The show’s hosts, Gaetano Kagwa & Eve D’Souza will reveal a weekly score-card that will keep track of what acts or performers came out tops in the popularity polls.
The top three stars will get a chance to share the stage with international artists at a mega concert scheduled for later in the year.
Tusker All Stars is part of Tusker’s continued commitment to nurturing musical talent and live music in the East African region.
The show is the second music reality TV show sponsored by the brand with the fifth season of East Africa’s first home grown music reality show, Tusker Project Fame expected to kick off later in the year. Take a look below;
JE, wewe ni mwanamume unayeshabikia au kupenda busu la mdomo? Kwa Kiswahili cha mitaani: Je, unapenda kula denda na mpenzi wako kila dakika?
Kwa wale wenye “ugonjwa” huo, basi mtafute mwenza wako mwenye ulimi mrefu, ni dhahiri utafurahia kamchezo hako!

Kama una uwezo, nakushauri umtafute kimwana Annika Irmler (pichani juu) ambaye ni raia wa Ujerumani.  Msichana huyo ambaye sasa ana umri wa miaka 16 ndiye mwanamke mwenye ulimi mrefu zaidi duniani kwa mujibu wa Kitabu cha Rekodi za Dunia za Guinness.

Binti huyo ambaye alivunja rekodi hiyo mwaka 2007 ni mwanafunzi wa sekondari, wakati huo akiwa na umri wa miaka 12.

Kwa ufahamu zaidi, mrembo Annika ana ulimu wenye urefu wa sentiminta 7.6.  Utakuwa huna ubishi kama utatazama picha inayoonyesha kipimo hicho.

Kwa kina mama wanaoshabikia ndimi ndefu za kina baba wafuatilie katika safu hii kila mara kwani watapata  kitu roho inatamani – tutawaletea mwanamume anayeshikilia rekodi ya kuwa na ulimi mrefu kuliko wanaume wengine duniani.

Ujumbe kwao (kina mama) utakuwa ni uleule: Kweli, tamu ya busu ni ulimi!
Hata hivyo, kwa mwanamume anayemtamani au kumtaka Annika itabidi asubiri amalize kwanza masomo yake kabla ya kutuma maombi ya kuwa naye bega kwa bega.

Annika anasema: “Sijui sana kuhusu ndimi, huenda ulimi wangu ukaendelea kurefuka.  Hata hivyo, nafurahi walimwengu wengi wananifahamu sasa kupitia ulimi huu.”

Kwa kina kaka na kina dada wanaopenda kurefusha ndimi zao, nafikiri teknolojia ya sasa inawezesha hivyo, kwani kuna utaalam mwingi tu wa kukuza viungo vingi vya mwili.
Kujaribu si vibaya, kwani kutojaribu ni kushindwa tayari.

MAAJABU JAMANIIIIIIII.....!

JE, umewahi kuona bilula “inayotema” maji bila kuliona bomba lake linakotokea?
Kwa ufahamisho tu ni kwamba, “bilula” ni kile kidude kilicho mwisho wa bomba linalobeba maji ambacho hutumiwa kulifunga au kulifungua ili liweze kutoa maji.

Neno hilo ni  Kiswahili murua japokuwa cha zamani.
Turejee kwenye swali letu: Umewahi kuliona bomba (bilula) linalotoa maji bila kujua au kuyaona maji hayo yanatokea wapi?

Kama hujawahi kuliona, basi ni hilo linaloonekana katika picha hii.  Bilula hiyo iko sehemu inayoitwa Aqualand, Hispania,  ni moja ya vivutio vikubwa duniani ambapo watu hufurika kwenda kushangaa.  Ni kivutio cha utalii.

Dude hilo ni kubwa na refu kwenda juu ambalo “hutema” maji kwa wingi kama vile yafanyavyo mabomba lukuki, kwa mfano, jijini Dar es Salaam, ambayo hunyonya maji kutoka Mto Ruvu ulioko mkoani Pwani.

Kweli, ni uchawi wa mchana kweupe!
Hata hivyo, ukweli ni kwamba: Hapa hapana uchawi wowote.   Katika sehemu inayotoa maji kuna bomba lililofichwa na maji hayo ambalo hunyonya maji hayo kutoka chini, likayarushwa juu halafu yakateremka tena kama vile “yanatemwa” na bilula hiyo!

Inafurahisha, au siyo?  Si uchawi, hata wewe unaweza kufanya hivyo!  Ni uchawi wa kisomi.
STAA wa Kibongo aliyejinyakulia umaarufu mkubwa kupitia ngoma ya Hands Across The World, Ali Saleh Kiba ‘Alikiba’ amepata ajali ya gari na wacheza shoo wake eneo la Mikumi, Morogoro wakiwa safarini kurejea jijini Dar es Salaam kutokea Mkoani Mbeya walikoenda kupiga shoo, Erick Evarist ana data kamili.

Kwa mujibu wa Alikiba, ajali hiyo ilitokea juzi Jumapili alfajiri (saa 11) ambapo gari dogo walilokuwa wakisafiria lilipinduka na kuacha njia eneo la Mikumi, hali iliyosabisha abiria nane waliokuwa ndani yake kujeruhiwa vibaya.
Hata hivyo, hakuna aliyepoteza maisha kwenye ajali hiyo na Alikiba alipata majeraha madogo huku baadhi ya wacheza shoo wake wakipata majeraha makubwa na kukimbizwa hospitali.

“Nahisi chanzo cha ajali ni dereva kusinzia kwani sote tulikuwa tumelala, tukashtukia gari likiacha njia na kupinduka. Namshukuru Mungu wote tumesalimika. Mimi sikuumia sana ila wenzangu walijeruhiwa na kukimbizwa kwenye Hospitali ta Mkoa wa Morogoro, mpaka sasa wote wamesharuhusiwa baada ya kupata matibabu na hali zao kuwa nzuri,” alisema Ali Kiba.
Na Shakoor Jongo
Ikiwa ni zaidi ya miaka miwili tangu walipofunga ndoa ya kihistoria, watayarishaji na waigizaji wenye majina makubwa Bongo, Wastara Juma (pichani) na Juma Kilowoko ‘Sajuki’, wamefunguka juu ya changamoto za kimaisha walizopitia katika kipindi hicho huku mwanadada huyo akiahidi kuzaa mapacha.

Akizungumza ‘exclusively’ na The 5Star Paper, Risasi Jumamosi juzikati akiwa njiani kuelekea visiwani Zanzibar ‘kushuti’ filamu yao mpya inayokwenda kwa jina la Kijacho, Wastara aliweka kweupe kwamba, ahadi aliyowekeana na mumewe katika ndoa yao imetimia hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula wa kupokea mgeni au wageni.

Wastara alisema kuwa, baada ya kufunga ndoa waliingia kwenye misheshe na msoto uliojaa changamoto za kimaisha za kutafuta ‘mahela’ ili kuweka mambo safi kabla ya kupata watoto lakini kwa sasa mambo yametulia na muda si mrefu ndoa yao ‘itatema’.

Alisema: “Jamani katika maisha ya ndoa si kweli kwamba watu wakishaoana wanakimbilia kuzaa, lazima wajiwekee malengo kwanza.
“Watu wanapaswa kujua kuwa, ni muhimu kuandaa mazingira ya huyo mtoto mwenyewe atakayezaliwa.

“Kwa sasa ni ‘full uhakika’, ninaamini haitafika Januari, mwakani na nadhani watakuwa ni watoto mapacha.
“Cha msingi tumuombe Mungu tu kwani muda wowote kuanzia sasa mashabiki wangu watasikia habari mpya za ndoa yangu.”

Baada ya kupata habari hizo njema kutoka kwa wastara huku ikiaminika kwamba kama Januari haitafika, basi malkia huyo wa filamu inawezekana ni mjamzito, Risasi Jumamosi lilimgeukia mumewe Sajuki na kumuuliza kuhusu suala hilo ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Natamani habari hizo za mke wangu kupata mapacha zitimie kwani itapendeza sana wakiwa wa kike na wa kiume.

Sajuki alisema, alipanga kuwa na mahali pake pa kuishi na usafiri wa uhakika hivyo kwa sasa amepata nyumba na gari kwa hiyo kilichobaki ni kusubiria watoto.
Wawili hao walifunga ndoa Mei, 2009 hivyo Mungu akiwajalia watoto mapacha watakuwa wamefunga kazi kwa mastaa ambao wameoa au kuolewa na
Jamii itambue kuwa mtu anayejifanya mpole kitandani hawezi kufanikiwa. Mwisho atamboa mwandani wake. Mantiki ya kutokuwa na muwajibikaji, hujenga tafsiri upande wa pili kwamba hujisikii inavyotakiwa, au huna hamu ila unatenda kwa kulazimisha.

Mzuka wa kutosha ni kitu muhimu mno unapokuwa faragha. Ndipo mwenzi wako anapoweza kuona mpo pamoja na akaamini kuwa unamtosheleza. Atajuaje kama anakupa raha stahiki ikiwa mwenzako anawajibika wewe umetoa macho kama mjusi kabanwa na mlango?

Hivyo basi, busara ya kwanza ya kitanda iwe ni kuziweka hisia zako kwenye tendo. Akikushika nawe shikika. Usizuie hisia, hebu tekenyeka basi. Unajikausha ili uonekane mgumu, nani alikwambia ugumu una nafasi pale wawili wanapokutana faragha?

Ukweli ni kuwa sanaa ya mapenzi inamuongoza mtu kujua maeneo gani ya kufanyia kazi. Kwa maana mpenzi wako atataka ayabaini maeneo ambayo wewe hukupa mzuka wa kutosha. Sasa atayajuaje kama unajikausha. Unaguswa mahali, wewe unakakamaa mwili mzima ili usioneshe hisia.

Ni mapenzi siyo mateso. Ni mchezo wa kugawana hisia. Mgawie zako naye akugawie zake. Usizibane, ukifanya hivyo utafeli. Mpe urahisi wa kutambua maeneo ambayo yanaweza kukupa raha, naye afanye hivyo kwako ili muweze kwenda sawa.

Winston Churchill, Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, aliyeongoza katikati ya karne ya 20 alisema: “Hakuna binadamu mwenye mafanikio kijamii aliyekosa ‘kashkashi’.” Akasisitiza, mtu ambaye anaishi kwa unyenyekevu na utakatifu akakosa dhambi yoyote, huyo mara nyingi anakuwa hana mchango kwa jamii.

Alimaanisha kiongozi mzuri nyuma ya pazia pengine ni mlevi kupita kiasi. Ana dorasi ya kupenda watu barabarani na kutaka kuingia nao kitandani. Kauli yake naichukua katika eneo kuwa kama hakuna binadamu aliyefanikiwa kijamii lakini akakosa ‘kashkashi’. 

Hata kitandani, inabidi uwe na kashkashi. Uoneshe ni kwa namna gani kinachotendeka eneo la tukio kinakuhusu. Tunapaswa kuheshimu wenzi wetu na siyo kuwa wapole.
Unyenyekevu faragha ni kutii kinachofanyika lakini siyo upole, pia papara haihitajiki.

Tunahitaji kutibu papara. Tunapaswa kuitambua miili yetu halafu twende na kasi tunayoimudu. Tuache kujipa mizigo tusiyoiweza. Wengi wanakwenda kwa waganga wa jadi wakidhani wanaumwa kumbe ni wazima.

Laiti kila mtu atakuwa mtulivu na kuheshimu hisia zake, naamini waganga wanaotengeneza fedha kwa kuuza dawa za mapenzi au nguvu za kiume wangefulia. Lakini wanapewa jeuri na watu wanaojiuguza ugonjwa wasiokuwa nao.

Zoezi la faragha linatekelezwa kwa nafasi na kituo, si kurukaruka. Umefika mshindo mara hii, baada ya sekunde kadhaa unajing’ang’aniza kurejea ulingoni. Unadhani kwa kufanya hivyo huyo uliyenaye atakuona upo ngangari. Unajidanganya.

Matokeo yake, badala ya kukuona ngangari ndiyo kwanza unaumbuka. Mwili haukuwa tayari kwa tendo, kwa hiyo papara zako zinakufanya ukutese. Unajitesa mwenyewe. Nyama choma ipo mbele yako, unaitamani lakini jeuri ya kuila huna. Aibu!

EPUKANA NA AIBU HII
Achana na simulizi za kijiweni. Usiendeshwe na tamaa. Himili wasiwasi halafu jiamini kwa kila nukta kisha utaona jinsi unavyoweza kutekeleza shughuli ipasavyo. Zingatia kuwa mapenzi yanahitaji muda wa kutosha. Ukitaka kurudi mara mbili ndani ya dakika 15 ndiyo mwanzo wa kuumbuka.

Mtu bora ni Yule anayechukua muda kufika mshindo mmoja, halafu anapumzika kwa muda wa kutosha kabla ya kurejea ulingoni tena. Umekutana naye, mara dakika tatu umecheua, kabla hujajipanga unataka upande tutani tena. Utachekwa kila siku.
Mapenzi hayakuumbwa ili umkomoe mwenzako.   

Itaendelea wiki ijayo.
London, England
David Beckham na mkewe, Victoria ‘Posh’, wanaotarajia kupata mtoto wa kike leo (Jumatatu, Julai 4, 2011), taarifa za ndani zinasema kuwa, kipindi chote cha ujauzito kilikuwa shwari kwa sababu ilikuwa ‘full kudekezana’.

Wiki iliyopita, gazeti moja nchini England liliripoti kuwa, Becks aliye staa wa soka wa England anayekipiga katika Klabu ya LA Galaxy ya Marekani, amekuwa akimfanyisha mazoezi mbalimbali mkewe ili yamsaidie kipindi cha kujifungua.
Akijifungua salama, huyo atakuwa mtoto wa nne wa Becks lakini wa kwanza wa kike, wanaye wengine ni Brooklyn (12), Romeo (8) na Cruz (6).

Habari zinasema kuwa, wenzi hao wamepanga kumpa mtoto huyo jina la Atlanta. (Picha iliyotumika hapo juu, ilitumiwa na gazeti hilo la Uingereza lakini si halisi bali imetengenezwa na mpiga picha Alison Jackson ili kuweka mazingira yanayofanana na hali halisi)

WEMA SEPETU


Na Mwandishi Wetu
Afya ya Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ina tatizo, mwili wake umetoa majibu na daktari amethibitisha.

Uchunguzi umebaini kuwa Wema anasumbuliwa na ugonjwa unaoitwa Adiposis Edematosa au kwa jina lingine ni Cellulite ambao chanzo chake mara nyingi husababishwa na mpangilio mbovu wa chakula.

Ngozi ya Wema ina mistari mingi hasa mgongoni lakini amekuwa hajui hali hiyo, ndiyo maana anashindwa kujisitiri na kuvaa mavazi yanayomuanika maeneo yaliyoathirika.
Chanzo cha Cellulite ni mabadiliko katika usagaji wa chakula, tatizo ambalo huwakumba wanawake wanaojiachia, hivyo Wema ameingia kwenye kundi hilo.

Kwa ufafanuzi zaidi wa kisayansi, ugonjwa huo pia chanzo chake ni matatizo katika mmeng’enyo na usanisi  wa chakula tumboni, ulaji wa kupindukia wa vyakula vigumu vyenye kemikali zinazoshambulia mfumo wa utengenezwaji wa seli za ngozi.

Cellulite pia ni matokeo ya mabadiliko ya ufanyaji kazi wa homoni za kike ambazo husababisha  ngozi kukunjamana, sababu za kijenetiki na mzunguko hafifu wa virutubisho vya ngozi kwenye damu.

Kuishi na msongo wa mawazo na hofu za mara kwa mara ni sababu nyingine inayochochea uzalishwaji wa kemikali iitwayo Catecholamines ambayo ikisambaa mwilini husababisha tatizo hilo.

DALILI
Kwa mujibu wa Daktari Abdullah Masoud ambaye amebobea katika tiba ya ngozi, dalili kubwa ya Cellulite ni mwili wa mwanamke kushambuliwa na mistari au mikunjo kwenye maeneo ya mgongoni, mapajani, mikononi na mengineyo.

“Ukishaona mistari juu kwenye mwili wa mwanamke maana yake tishu zake zimeshaharibika na kupoteza mpangilio wake wa kawaida (dimorphic skin architecture), kwa hiyo mara kwa mara huwa tunawashauri wanawake waangalie mpangilio wa maisha yao kwa jumla,” alisema Dokta Masoud.

Aliendelea: “Siyo mistari tu, hilo naomba lieleweke, hata mikunjo ya ajabu ajabu kwenye mwili wa mwanamke hasa kijana ni matokeo ya Cellulite.”

Dk. Masoud alisema: “Unywaji wa pombe kali, uvutaji wa sigara navyo ni tatizo. Naomba wanawake waache, wanaharibu ngozi zao.”

WEMA HAJIJUI 
Ijumaa Wikienda limebaini kuwa Wema hajui kuhusu tatizo hilo ndiyo maana amekuwa akivaa mavazi yanayoacha wazi sehemu za mgongo wake ambayo ndiyo uliyoathirika zaidi.
Limebaini pia kuwa Wema ameathirika hata kwenye maungio ya mikono na mabega pamoja na sehemu ya kifuani.
WEMA ZAMANI BWANA!
Gazeti hili baada ya kuona picha za Wema aliyeharibika, lilirudi kujiridhisha kwa kuangalia zile za zamani na kubaini kwamba alikuwa ‘kifaa cha nguvu’ na sasa ni ‘fotokopi’.

Ngozi ya Wema wa zamani ilikuwa laini inayovutia, haikuwa na mistari wala mikunjo, hivyo kumfanya awe mrembo anayestahili kuvuliwa kofia.

WEMA ANAWEZA KUPONA?
Tiba kadhaa zimekuwa zikitajwa kumaliza tatizo hili ingawa wataalamu wameshindwa kuthibitisha ufanisi wake.

Kwa mujibu wa Dokta Masoud, hakuna tiba ya uhakika ya kumaliza tatizo hilo ingawa zipo baadhi ya dawa ambazo zinatajwa kupunguza makali ya Cellulite.

“Mpaka sasa hakuna tiba ya moja kwa moja ya Cellulite ila inashauriwa kwa mtu mwenye tatizo hilo abadili mfumo wa maisha yake na akifuata m
Na Musa Mateja
HE! Mhusika rasmi katika ‘industry’ ya filamu za Kibongo, Wema Abraham Sepetu (pichani) ametoa kauli iliyojaa mshtuko kuwa, anajipanga kugombea ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.

Akizungumzia na ‘The Five Star Paper’, Risasi Jumamosi ndani ya Hoteli ya The Atriums iliyopo Sinza-Afrikasana, Dar es Salaam juzikati, Wema ambaye ni Miss Tanzania 2006/07 alisema kuwa, katika mipango na ndoto zake za miaka minne ijayo, ni pamoja na kugombea nafasi ya ubunge.

Wema alifunguka kwamba, nyuma ya mpango huo kuna baba yake ambaye aliwahi kutumikia siasa kwa ngazi ya kidiplomasia ikiwa ni pamoja na kuwa balozi ambaye amekuwa akimshauri mara kwa mara kujikita kwenye kilinge cha siasa.
“Mwazo nilikuwa silifikirii sana jambo hilo, lakini baba amekuwa ‘akini-inspire’ mno.
“Nimeshaanza maandalizi kuelekea 2015, naomba Watanzania wanipe sapoti,” alisema Wema.
Alipoulizwa chama na jimbo atakalogombea, Wema alisema:

“Kuhusu chama nitaangalia kitakachokuwa na nguvu hadi kufikia 2014. Jimbo nitakalogombea bado nalitafiti hivyo nitaliweka hadharani ‘leita’.”

Wema ambaye kwa sasa ‘anatoka’ kimapenzi na msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’ amekuwa akikumbwa na skendo za hapa na pale lakini sasa ameahidi kubadilika ili kujijenga kisiasa.
Na Shakoor Jongo
CD na VCD zinazomuonesha mshiriki wa Big Brother Amplified 2011, Bhoke Egina akifanya malavidavi na aliyekuwa mwakilishi  wa Uganda, Ernest Wasake imeanza kusambazwa na wafanyabiashara wa mitaani ‘Wamachinga’ jijini Dar es Salaam,” Risasi Jumamosi lina data kamili.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umegundua kuwa Wamachinga wanauza CD hizo kati ya shilingi 2500 na 3,000 na kuzifanya zigombewe kama peremende.

Gazeti hili liliongea na baadhi ya watu walioziona CD na VCD hizo zikiuzwa katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam ambao pia walishangazwa na vitendo alivyofanya binti huyo katika Jumba la Big Brother, Afika Kusini.

“Tulikuwa tukisoma kwenye vyombo vya habari lakini hatukuamini kama ni kweli Bhoke amefanya uchafu ule na raia wa Uganda,” alisema Mama Jumaa, mkazi wa Magomeni jijini Dar.
 “Mimi sina ‘king’amuzi’, nimeona katika CD hii, sasa najiuliza hivi alivyokuwa akifanya uchafu ule wazazi wake na ‘boyfriend’ wake walikuwa wakiangalia?” alisema mtu mwingine ambaye jina lake halikupatikana  mara moja.
Baada ya kusikia kauli hizo, Risasi Jumamosi liliwavutia waya baadhi ya mastaa wa Bongo ili kusikia maoni yao kutokana na kitendo hicho alichokifanya Bhoke.
Mcheza filamu maarufu, Vincent Kigosi ‘Ray’: “Nahisi katudhalilisha sana Watanzania, lakini kwa upande mwingine siwezi kumhukumu kwa sababu sina uzoefu wa nyumba ya Big Brother, inawezekana mazingila yanamruhusu kufanya uchafu ule lakini ni bora aliyoyafanya Lotus kuliko uchafu wa Bhoke,”alisema.

Aidha, Ray aliwashauri wawakilishi wa Big Brother nchini kuachana na kuwapeleka akina dada katika mashindano hayo, kwa kuwa hawana historia nzuri tofauti na wanaume.
“Habu angalia alichokifanya Richard Bezuidenhout na Mwisho Mwampamba ambao waliweza kulitangaza vyema taifa,”alisema.

Staa mwingine wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ yeye alisema kitendo alichokifanya Bhoke kimemsikitisha sana kiasi na kuona aibu kama vile amekifanya yeye.
“Kwa kweli Bhoke ametuvua nguo, ule si utamaduni wa mwanamke wa Kitanzania, nilitegemea alivyorudi angeomba radhi, matokeo yake anasema alienda Big Brother kama Bhoke na siyo kuipeperusha bendera ya Tanzania, inasikitisha,”alisema.

Staa mwingine wa filamu, Aunt Ezekiel yeye alikuwa tofauti kidogo pale aliposema kuwa kimaadili ya Kitanzania Bhoke amekosea lakini anayachukulia matendo aliyoyafanya kama ni njia ya kusaka ushindi.
“Sitaweza kumchukia, kwani nahisi alivyokuwa mjengoni alikuwa siyo Bhoke yule tunayemjua siye, kwa hiyo nikibahatika kukiona kipindi chake nitamchukulia kuwa ni mtangazaji na nitakaa na kukiangalia bila ya ‘kumjaji’ vibaya,” alisema.

Staa wa filamu, Mwanaidi Suka ‘Mainda’ alisema: “Kwa kweli siwezi kuongea chochote, kwani sikubahatika vitendo vyake, nitakuwa kama nahukumu kitu nisichokijua, kitendo ambacho ni dhambi mbele ya Mungu.”

Mtangazaji wa Radio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’: “Kama kuna watu wanamchukia Bhoke, basi mimi ni namba moja, kitendo chake kimetudhalilisha, halafu inaonesha ni mwepesi kwa mwanaume na bingwa wa kutongoza, unajua Bhoke ndiye aliyejitongozesha kwa Ernest? Eti mtangazaji, asituharibie fani yetu,” alisema.

Aidha, Dida alisema kuwa alifahamu kama CD na VCD za uchafu alioufanya zitauzwa na kuongeza kuwa haiwezi kuishia hapo, kwani hata kwenye simu watu wanahamishiana uchafu wake.
Mcheza filamu Jacqueline Pentzel  ‘Jack wa Chuz’:“ Amejidhalilisha, labda kama ni masharti aliyopewa na Big Brother afanye vile mi nitaona ni kawaida.”
Mwingine aliyechangia ni mcheza filamu maarufu, Rose Ndauka: “Kanichefua sana, sijui amelelewa vipi, ningekuwa miye yaani hata nyumbani nisingepokelewa,” alisema.
Msanii huyo alisema kuwa bado hajaiona CD ya uchafu wa Bhoke na kuongeza kama kweli itakuwepo, itakuwa ni aibu yake kwa mara ya pili.
Staa wa filamu, Latifa Idabu ‘Badra’: “Mimi namuona mshamba tu hana lolote, ametudhalilisha sana, umaarufu hautafutwi kama vile.”

Msanii mwingine wa filamu, Zuwena Mohammed ‘Shilole’:” Mi siwezi kusema chochote.”
Akihojiwa na Jarida la iMagazine la Uingereza hivi karibuni, Bhoke alisema: “Siku ile nilikuwa nimelewa sana hivyo siwezi kubisha kilichotokea.” 
Na Shakoor Jongo
Wimbi la baadhi ya masupastaa wa Bongo kuzaa watoto bila kuwa kwenye ndoa au kuishi na mwanamume, sasa limeonekana kuwa fasheni huku wengi wao wakiwa wanawaficha waliowapa ujauzito, Risasi Jumamosi limebeba mkoba wa uchunguzi.

Utafiti wa kina umeonesha kwamba, baadhi ya mastaa hao wamekuwa wakibeba ujauzito bila kujali wanamume wanaowapa, ili mradi awe na mshiko.

Katika tafsiri ya kiimani kutoka kwenye vitabu vitakatifu, mastaa hao wanazini kwa vile, maandiko yanaelekeza kuwa, mwanamume au mwanamke anatakiwa kufunga ndoa kabla ya kujamiiana.

Kwa mujibu wa msanii mmoja anayeshika kasi kwenye gemu la maigizo kwa sasa Bongo (jina tunalo), mastaa wengi wa kike wameamua kuzaa bila ndoa kwa sababu wanaume wa kuwaoa hawapo na wao umri unakwenda.

Akiendelea kuweka wazi siri hiyo ya mastaa kuzaa kwa fasheni, msanii huyo alisema kuwa, pia wapo mastaa ambao wanaamua kunasa mimba ili kujihakikishia kwamba wao si wagumba.

“Wapo (mastaa) waliamua kubeba mimba ili kujipima kama wazima au tasa, lakini wengine ni wale ambao umri umekwenda lakini hawaolewi, nao wameamua kuzaa ili wawe na watoto japo wa dawa,” alisema msanii huyo.
Risasi Jumamosi lina orodha ya mastaa wa Bongo ambao wamezaa bila kuolewa na wengine wakiwaficha ‘mababa’ wa watoto wao.
Maureen Gislary; Mshiriki wa Miss Tanzania mwaka 2005, mwaka huu alijifungua mtoto wa kike aitwaye Milania Fiona huku akikataa katakata kumwanika mzazi mwenzake.

Suzana Chubwa ‘Queen Suzy’; Ni mnenguaji wa Bendi ya FM Academia. Ana mtoto mmoja aitwaye Jackson Junior ambaye inasemekana alizaa na muimbaji wa Bendi ya Mapacha Watatu, Kalala Hamza ‘Junior’. Baba huyo aliwahi kumkataa mtoto. Hawapo katika ndoa.
Nancy Sumari; Miss Tanzania mwaka 2005 (pichani), amejifungua mwaka huu mtoto wa kiume. Naye amekataa kabisa kumtaja baba wa mwanaye akisema ni siri yake, lakini hajaolewa.

Snura Mushi; Ni msanii wa filamu za Kibongo, ana mtoto wa kike aitwaye Talha aliyejifungua mwanzoni mwa mwaka huu. Yeye pia hajawa wazi kumwanika baba wa mtoto wake huyo akisema ni siri yake. Hayuko kwenye ndoa.

Husna Iddi ‘Sajenti’; Ni Kimwana Manywele 2008. Yeye ana mtoto wa kike aliyezaa na mwimbaji wa Bendi ya The African Stars, Charles Gabriel ‘Chalz Baba’. Mtoto anaitwa Carinal Charles Gabriel.

Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’; Yeye ni staa waTamthiliya ya Jumba la Dhahabu. Amezaa mtoto mmoja na msanii mwenzake, Tuesday Kihangala ‘Mr Chuz’. Hawako kwenye ndoa na wala hawakuwa na mpango wa kuoana.

Isabella Mpanda ‘Bellah’; Ni Miss Ruvuma 2008. Alijifungua mtoto wa kiume mwaka 2010 na kumwita Obama. Amewahi kutamka kuwa, baba wa mtoto wake ni kigogo wa Wizara ya Ujenzi jijini Dar es Salaam, lakini amekuwa akikataa kumtaja jina.

Joyce Kiria; Presenta wa Vipindi vya Bongo Movies na Wanawake Live. Mwezi Juni, 2011 alijifungua mtoto wa kiume kwa njia ya upasuaji akiwa ameachika kwa mumewe, Nelson Nkongo ‘Dj Nelly’. Kwa sasa ana mchumba lakini haijajulikana lini atafunga ndoa.

Lucy Komba ‘Lona’; Ni staa wa filamu Bongo, ana mtoto aitwaye Strom. Tofauti yake na baadhi ya mastaa wenzake wenye watoto, yeye anamtaja Francis Mbasha kuwa ndiye baba wa mtoto huyo. Lakini hawaishi pamoja na wala hawana mpango wa kufunga ndoa.

Aisha Mohamed Mbegu ‘Madinda’; Ni mnenguaji wa Bendi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta’. Licha ya kuwa na watoto wawili, kila mmoja na baba‘ake, hivi karibuni alitamka kuwa, anataka kuzaa mtoto mwingine, lakini hajaolewa.